Habari za Yanga
Habari za michezo

UKWELI KUHUSU KIUNGO MPYA WA YANGA HUU HAPA….ISHU YA FEI TOTO YATAJWA TENA..

admin December 14, 2023 2:29 pm

UONGOZI wa Yanga umekamilisha usajili wa kiungo wa JKT FC na timu ya Taifa ya vijana Zanzibar, Shekhan Ibrahim kujiunga na kikosi cha timu kipindi cha usajili wa dirisha dogi linalotarajiwa kufunguliwa mapema mwezi huu.

Taarifa kutoka Yanga kuwa tayari wamemalizana na kiungo huyo baada ya kuridhishwa na uwezo wake na kuwafanya viongozi kuvutiwa na kumsainisha mkataba.

Mtoa habari huyo ameeleza kuwa baada ya kufanikiwa kumuuza Feisal Salum kwenda Azam FC, sasa wamefanikiwa kupata mbadala wake ambaye ni Shekhan.

Alipotafutwa Katibu Mkuu wa JKU ya Visiwani Zanzibar, Shadhil khatib alisema nyota huyo kwa sasa sio mali yao baada ya kukamilisha usajili na klabu ya Yanga kwa kusaini mkataba wa miaka mitatu.

Amesema kwa upande wao wamemalizana na Yanga baada ya makubaliano ya uhamisho wa kiungo huyo ambaye ukifika muda Yanga watamtambulisha.

“Ni kweli kwa sasa Shekhan sio mchezaji wetu kwa sababu amesaini mkataba wa miaka mitatu na tumeshamalizana na Yamga kuhusu uhamisho wa nyoya wetu huyo,” amesema Katibu huyo.

Shekhan ni moja ya viungo bora vinana wanachipukia kwa sasa ndani ya soka la visiwani Zanzibar, mwenye ubunifu mkubwa akiwa uwanjani na ni moja ya viungo wenye mashuti makali sana.

BENCHIKHA ASHUSHA MASHINE YA KAZI SIMBA ACHANA NA CHASAMBI….KIFAA HIKI KIPYA KUTOKA MOROCCO NACHO KINATUA MSIMBAZI…

Deprecated: File Theme without comments.php is deprecated since version 3.0.0 with no alternative available. Please include a comments.php template in your theme. in /home/sokalabo/public_html/wp-includes/functions.php on line 6170

Leave a Reply