Habari za michezo

DOH GUARDIOLA NDIO BASI TENA MAN CITY

Staff Desk December 24, 2023 12:25 pm

Meneja wa Manchester City, Pep Guardiola amesema “amefunga ukurasa” katika klabu hiyo ya Ligi ya Premia baada ya kushinda Kombe la Dunia la Vilabu.

City ilishinda Fluminense 4-0 siku ya Ijumaa na kunyanyua taji lao la tano la 2023.

Ilimaanisha Guardiola ameshinda kila taji lililopo tangu alipojiunga kama meneja mnamo 2016.

Akizungumza baada ya mchezo huo, Guardiola, ambaye amebakiza miezi 18 katika mkataba wake, alisema kazi yake “imekwisha”.

Alisema: “Nimefurahishwa sana na ningependa kusema tulikuwa na hisia kwamba tutafunga ukurasa; tulishinda mataji yote, hakuna kitu kingine cha kushinda. Nilikuwa na hisia kwamba kazi imekamilika, imekwisha.

“Sasa ni wakati wa Krismasi, tunanunua kitabu kingine na kuanza kukiandika tena. Miaka minane iliyopita, imekwisha.”

MWAMNYETO ALIANZISHA YANGA… ATAKA KUTUMKIA HUKU YANGA FUNGA MWAKA INAFANYIKA HIVI

Deprecated: File Theme without comments.php is deprecated since version 3.0.0 with no alternative available. Please include a comments.php template in your theme. in /home/sokalabo/public_html/wp-includes/functions.php on line 6170

Leave a Reply