Habari za Yanga
Habari za michezo

HUU HAPA USAJILI MPYA YANGA …ENG HERSI AUNGANISHIWA DILI AKIWA PSG….

admin January 9, 2024 5:42 pm

IMEFICHUKA kuwa, Rais wa Yanga Injinia Hersi Said ameenda Ulaya akiwa na hesabu za kukamilisha usajili wa kushtua iwapo atafanikiwa kumnasa straika anayecheza soka barani humo.

Yanga imebakiza mastaa wawili tu wa kuongeza kikosini akiwamo winga wa maana wa kulia huku hesabu zao zikiwa kwa Agee Basiala wa Union Maniema ya DR Congo ambaye tayari ameshatumiwa mkataba wa miaka miwili.

Hesabu za Yanga zilizosalia ni kufanya usajili wa mshambuliaji wa kati mwenye ubora na hapo ndipo ikafahamika kwamba Hersi atashuka na mtu.

Hersi alikuwa Ufaransa kwa ziara ya mualiko na mabosi wa klabu kubwa ya Paris Saint German (PSG) lakini ndani yake kuna hesabu za usajili.

Inaelezwa Hersi atakutana na viongozi wa klabu moja ya Asia waliopo Ufaransa kuangalia uwezekano wa kumnasa mshambuliaji mmoja.

Yanga inataka kuwa na mshambuliaji ambaye atawasaidia sasa kwenye msimu huu kwenye Ligi ya Mabingwa Afrika.

“Tunahitaji mshambuliaji wa kati na na kuhakikishia Hersi hatarudi patupu, atashuka na mshambuliaji wa maana wa kuipa ubora timu,” alisema bosi wa juu wa Yanga.

SIKU CHACHE BAADA YA KUTANGAZWA… BENCHIKHA KAIBUKA NA HILI KUHUSU USAJILI WA SARR… KUHUSU KUSAJILIWA NA YANGA…MSUVA AVUNJA UKIMYA….AFUNGUKA MSIMAMO WAKE….

Deprecated: File Theme without comments.php is deprecated since version 3.0.0 with no alternative available. Please include a comments.php template in your theme. in /home/sokalabo/public_html/wp-includes/functions.php on line 6170

Leave a Reply