Habari za Michezo leo
Habari za michezo

SIMBA, YANGA ZILIVYOPELEKA KILIO NA KUVURUGA TIMU ZA WAARABU….HAWAAMINI KABISA…

admin March 6, 2024 11:42 am

Tangu mwaka 2014, walau timu moja kutoka Algeria au Morocco zilifanikiwa kuingia kwenye hatua ya robo fainali ya Ligi ya Mabingwa barani Afrika, lakini rekodi hiyo imeharibiwa na Simba na Yanga ambazo msimu huu zimekwamisha timu kutoka mataifa hayo kutinga robo fainali.

Simba iliizuia Wydad Casablanca iliyokuwa nayo kwenye kundi B, ambapo wote walikuwa na pointi tisa lakini Simba ikapita kwa faida ya matokeo bora ya ugenini pale timu hizo mbili zilipokutana. Simba ililala 1-0 kule Morocco lakini ikashinda 2-0 nyumbani Dar es Salaam.

Kwenye kundi lao tayari Asec Memosas ilishafuzu kwenda hatua ya robo fainali na ilitakiwa timu moja kati ya Simba, Wydad na Jwaneng Galaxy, lakini Simba ndio ilifuzu na kusababisha Morocco ishindwe kuingiza timu kwenye robo fainali kwani AS FAR ambayo ilishiriki ilitolewa kwenye hatua za awali.

Hiyo pia ilikuwa ni mara ya kwanza kwa Wydad kutolewa kwenye hatua ya makundi katika mara zote ilizowahi kushiriki michuano hii na kufika hatua hiyo.

Kwa upande wa Yanga pia mambo yalikuwa ni hivyo hivyo. Iliizuia Algeria isiwe na timu hata moja kwenye robo fainali ya michuano hii baada ya kuiondosha CR Belouizdad.

Belouizdad na Yanga ambazo zote zilikuwa kundi D, zilimaliza kundi kwa alama nane lakini Yanga ilikaa juu ya Waarabu hao wa Algeria kwa sababu ilipata matokeo mazuri kwenye mechi zao mbili za makundi walipokutana. yanga ilipasuka 3-0 katika mechi ya ufunguzi wa Kundi D dhidi ya Belouizdad kule Algeria kabla ya kuja kuichakaza 4-0 kwenye Uwanja wa Mkapa, Dar es Salaam.

Baada ya kutoka kwa Belouizdad, Algeria ikaambulia patupu kwenye hatua ya robo fainali kwa sababu mshiriki mwingine kutoka nchi hiyo CF Constantine alitolewa kwenye hatua ya awali na Etoile du Sahel.

Yanga iliungana na Al Ahly ambayo ilimaliza kinara wa kundi D kwa pointi 12.

PACOME ZOUZOUA AMFUNIKA CHAMA TAKWIMU ZA CAF….’DATA’ KAMILI HIZI HAPA… KIGOGO TFF AFICHUA UKWELI WA MKATABA WA DUBE NA AZAM FC…’HAKUNA MIL 700 ..SIASA TUPU…”

Deprecated: File Theme without comments.php is deprecated since version 3.0.0 with no alternative available. Please include a comments.php template in your theme. in /home/sokalabo/public_html/wp-includes/functions.php on line 6170

Leave a Reply