Rekodi Inavyoihukumu JKT Tanzania
WAKATI uongozi wa JKT Tanzania ukiguswa na kuomba radhi kwa mashabiki wa soka baada ya mchezaji wa timu hiyo, Hassan Wahabi kumfanyia rafu mbaya kiungo mshambuliaji wa Yanga, Pacome Zouzoua, rekodi zinawahukumu wachezaji wa kikosi hicho, kwani tangu kuanza msimu wa 2024-2025, hadi 2025-2026, ndiyo wanaoongoza kwa kuonyeshwa kadi nyekundu.
Katika mechi ya mwisho ya msimu wa Ligi Kuu ya NBC iliyochezwa Juni 30, 2026 kwenye Uwanja wa Meja Jenerali Isamuhyo, Dar wakati Yanga ikishinda kwa mabao 3-0, Wahabi alimchezea madhambi Pacome dakika ya 46 na kushindwa kuendelea na mechi hiyo iliyoipa Yanga taji la tano mfululizo. Majeraha hayo yamemfanya Pacome afanyiwe upasuaji na kutarajiwa kukaa nje kwa wiki sita.
Wachezaji wa JKT Tanzania wameonyeshwa kadi nyekundu sita za Ligi Kuu ya NBC, wakifuatiwa na TRA United na Pamba Jiji ambazo kila moja zimepata nne na KMC tatu.
Nyota mwingine ni Mohamed Bakari, katika kichapo cha bao 1-0 dhidi ya Simba, lililofungwa kwa penalti na Jean Charles Ahoua dakika ya 90+5, kwenye Uwanja wa KMC Complex, Desemba 24, 2024.
Msimu huu wa 2025-2026, nyota wanne wameonyeshwa kadi nyekundu, akianza pia kipa Ramadhan Chalamanda dhidi ya Mbeya City, Oktoba 24, 2025, katika sare ya 2-2.