Tetesi za Usajili
Habari za michezo

Vardo July 27, 2026 9:22 pm

Mabadiliko makubwa yanaonekana kumsubiri winga wa Paris Saint-Germain (PSG), Bradley Barcola (23), baada ya kutoa taarifa za kusitisha rasmi mazungumzo ya kuongeza mkataba mpya na mabingwa hao wa Ufaransa.

Mkataba wa sasa wa Barcola umebakiza miaka miwili, hali inayozidi kuchochea uvumi wa kuondoka kwake kutokana na kutoridhishwa na nafasi ya kucheza chini ya kocha Luis Enrique.

Kwa mujibu wa gazeti la L’Equipe, hatua hii imefungua rasmi vita ya usajili:

  • Liverpool: Inaonekana kuwa mbele zaidi kumpata winga huyo. Mradi wa kisoka chini ya kocha mpya Andoni Iraola unatajwa kumshawishi sana mchezaji huyo.

  • Arsenal: Inaendelea kumfuatilia kwa karibu.

  • Chelsea na Bayern Munich: Zinaonyesha nia, lakini inaarifiwa kuwa Barcola tayari amekataa mpango wa kujiunga na Chelsea.

PSG bado haijatoa tamko rasmi kama itamuuza msimu huu, kwani maamuzi yao yatategemea ikiwa watafanikiwa kumpata Yan Diomande wa RB Leipzig.


Real Madrid Yataja Bei ya Vinicius Jr

Real Madrid imeweka dau la euro milioni 160 (pauni milioni 137) kwa mshambuliaji wake hatari Vinicius Jr iwapo itatokea klabu inayotaka kumsajili msimu huu. Walio na nia kama Arsenal bado hawajawasilisha ofa rasmi, huku Mabingwa hao wa Hispania wakisisitiza kuwa hawatamruhusu kuondoka kwa ada ya chini ya hapo.


Bruno Guimaraes Aweka Shinikizo Newcastle United

Kiungo wa Brazil, Bruno Guimaraes, amewaeleza mawakala wake kuwa anataka mustakabali wake ujulikane ndani ya wiki moja kabla ya kuanza maandalizi ya msimu mpya. Arsenal inaendelea kufuatilia hali yake, ingawa Newcastle United bado haijaonyesha nia ya kuanza mazungumzo ya kumuachia.


Spurs Mbele Kumsajili Savinho Kutoka Man City

Tottenham Hotspur ipo kwenye hatua nzuri za kumsajili winga wa Brazil, Savinho (22), kutoka Manchester City. Mazungumzo yanaendelea vyema na Spurs ina imani ya kukamilisha usajili huo kabla ya msimu mpya wa Ligi Kuu England kuanza.


Yan Diomande Atengeneza Njia ya Kuelekea Real Madrid

Miamba ya Hispania, Real Madrid, imefikia makubaliano ya awali ya maslahi binafsi na winga chipukizi wa Ivory Coast, Yan Diomande (19), anayekipiga RB Leipzig. Sasa Madrid inajiandaa kuanza mazungumzo rasmi ya ada ya uhamisho na klabu yake.


Al-Hilal Yamtaka Iliman Ndiaye wa Everton

Klabu ya Al-Hilal ya Saudi Arabia imeanza mazungumzo ya kumsajili winga wa Senegal, Iliman Ndiaye (26), kutoka Everton kwa ofa nono. Everton inasubiri kuona kama dau hilo litakidhi matakwa yao kabla ya kuridhia uhamisho huo.


Chelsea Yaikazia Boti Pedro Neto

Chelsea haipo tayari kumuuza kwa urahisi winga wake Pedro Neto (26). Licha ya Liverpool, Manchester City na klabu za Saudi Arabia kuonyesha nia, mabosi wa Stamford Bridge wanaamini Neto bado ni sehemu muhimu ya kikosi chao kwa msimu ujao.


Besiktas Yamsubiri Mohamed Salah

Klabu ya Besiktas bado inasubiri uamuzi wa mshambuliaji wa Misri, Mohamed Salah (34), baada ya kumtumia ofa ya mwisho. Salah kwa sasa ni mchezaji huru baada ya kuondoka Liverpool na bado anatathmini hatua yake inayofuata.


Junior Kroupi Kusalia Bournemouth

Bournemouth haina mpango wa kumuuza mshambuliaji wake Mfaransa Junior Kroupi (20), licha ya kutakiwa na Barcelona. Klabu hiyo inamchukulia Kroupi kama mchezaji wa mradi wa muda mrefu.


Fulham Kupewa Kipao Mbele kwa Franco Mastantuono

Fulham ndiyo inayopewa nafasi kubwa ya kumpata kwa mkopo kiungo chipukizi wa Argentina, Franco Mastantuono (18), iwapo Real Madrid itaamua kumtoa kwa mkopo ili kupata uzoefu zaidi wa Ligi Kuu England.

Simba Yamtema Mohamed Bajaber, Karabaka Apelekwa Mkopo Pamba Jiji