WAFCON Kundi A
Habari za michezo

Vita ya Kileleni Kundi A! Morocco na Algeria Kukipiga, Kenya na Senegal Kusaka Pointi za Kwanza

Vardo July 30, 2026 10:08 am

Baada ya kumalizika kwa mzunguko wa kwanza wa hatua ya makundi katika Mashindano ya Kombe la Mataifa ya Afrika kwa Wanawake (WAFCON), leo macho na masikio ya wapenda soka yatakuwa kwenye mechi za pili za Kundi A zinazotazamiwa kuwa na ushindani wa hali ya juu.


1. Senegal vs Kenya (Saa 12:00 Jioni – Rabat Olympic Stadium)

Mchezo wa kwanza wa siku utazikutanisha timu za Senegal na Kenya, mchezo unaotajwa kuwa wa ‘pata au kosa’.

Timu zote mbili zilianza mashindano vibaya kwa kupokea vipigo katika mechi zao za kwanza:

  • Kenya ilikubali kichapo cha mabao 4-0 dhidi ya wenyeji Morocco.

  • Senegal ilipoteza kwa mabao 2-0 dhidi ya Algeria.

Matokeo hayo yanaifanya mechi hii kuwa na umuhimu mkubwa sana kwa pande zote mbili. Ushindi utairudisha timu mchezoni na kuipa matumaini ya kufuzu, huku kichapo kingine kikimaanisha safari ya kurejea nyumbani mapema.


2. Morocco vs Algeria (Saa 3:00 Usiku – Moulay El Hassan Stadium)

Mchezo wa pili utakuwa wa kukata na shoka kati ya wenyeji Morocco na majirani zao Algeria.

Hivi sasa, Morocco ndio vinara wa Kundi A wakiwa na pointi 3, sawa na Algeria, lakini wakiwa mbele kwa tofauti ya mabao ya kufunga na kufungwa.

  • Nini kipo hatarini? Timu itakayoibuka na ushindini katika mchezo huu itajihakikishia nafasi ya kutinga hatua ya robo fainali moja kwa moja.

  • Sare: Ikitokea sare, vita ya kusonga mbele itahamia kwenye mechi za mwisho za kundi hilo.


Rekodi na Takwimu za Hivi Karibuni

  • Morocco (Wenyeji): Wanaingia kwenye mchezo huu wakiwa na rekodi nzuri nyumbani na safu kali ya ushambuliaji iliyofunga mabao 4 dhidi ya Kenya (yakiwemo mawili ya Nahila Jrandi). Hii ni mara ya pili mfululizo Morocco wanaandaa WAFCON (baada ya 2022 walipofika fainali na kuwa taifa la kwanza kutoka Afrika Kaskazini kufanya hivyo).

  • Algeria: Hii ni ushiriki wao wa 7 katika historia ya WAFCON (wakishiriki miaka ya 2004, 2006, 2010, 2014, 2018, na 2024). Lengo lao kuu ni kuvunja mwiko wa kuishia hatua ya makundi na kutinga robo fainali.

Simba Day 2026: FC Lupopo Kutua Bongo Kuikabili Simba SC Agosti 8 Vipers SC Kutwaa Ubingwa CECAFA Kagame Cup: Kocha Lavagne Atoa Onyo!