Uncategorized

SAMATTA: KESHO TAIFA NI MWENDO WA BURUDANI, MASHABIKI JITOKEZINI KWA WINGI

admin June 1, 2019 11:14 am

NAHODHA wa timu ya Taifa, Mbwana Samatta amesema kuwa mashabiki kesho wajitokeze kwa wingi uwanja wa Taifa kutoa sapoti kwenye mchezo wa hisani dhidi ya timu ya Ali Kiba utakaochezwa majira ya saa 10:00 Jioni.

Akizungumza na SalehJembe, Samatta amesema kuwa wakati sahihi wa kujitoa kwa ajili ya jamii ni sasa hivyo wao wanaanza wengine watafuata.

“Ni mradi ambao upo kwa ajili ya jamii yetu, tunajua kwamba uhitaji ni mkubwa ila ni mwanzo mzuri, mashabiki wajitokeze kwa wingi kuona namna tutakavyowapa burudani na pia tunarejesha kile tunachokipata kwa jamii,” amesema Samatta.

Mradi wa Samata na Kiba umepewa jina la SAMAKIBA Foundation na ulianza mwaka jana ambapo walirejesha kwa wanafunzi wanaoshi kwenye mazingira magumu, msimu huu ni mara ya pili.

KIKOSI CHA LIPULI DHIDI YA AZAM FC LEO, ALIYESAJILIWA YANGA AANZIA BENCHI KIKOSI CHA AZAM DHIDI YA LIPULI

Deprecated: File Theme without comments.php is deprecated since version 3.0.0 with no alternative available. Please include a comments.php template in your theme. in /home/sokalabo/public_html/wp-includes/functions.php on line 6170

Leave a Reply