Uncategorized

CHIRWA AIFANYIA MAAMUZI MENGINE YANGA

admin June 6, 2019 9:00 pm


MAMBO yamemnyokea mshambuliaji wa Azam FC Obrey Chirwa baada ya kuelewana na kukubaliana kusaini mkataba wake mpya na klabu hiyo tukio ambalo litafanyika Jumamosi.

Awali Chirwa ambaye ni Mzambia ligoma kusaini mkataba mpya na klabu hiyo na inatajwa kuwa malengo yake yalikuwa ni kutaka kurejea Yanga lakini kocha Zahera akamkaushia.

Chirwa aliwahi kuichezea Yanga kabla ya kutimkia Misri kisha kurejea na kujiunga na Azam FC msimu huu katika ligi amefunga jumla ya mabao matatu.

Mratibu wa Azam FC, Philipo Alando alisema kuwa tayari wameongea na wachezaji kinachosubiri wa sasa ni kusaini tu na kuendelea na mambo mengine.

“Unajua kila kitu kina kwenda sawa Chirwa pamoja na wenzake tumeshaongea nao na kutakubaliana kilichokuwa kinasu biriwa ni wao kuweza kusaini mikataba yao na kundelea na mambo mengi,”alisema Alando ambaye ni mchezaji wa zamani wa Kagera Sugar na Azam.

Uwepo wa taarifa hizi unaleta ugumu wa Chirwa kurejea katika klabu yake ya zamani ambayo ni Yanga baada ya kuwepo kwa tetesi zilizoelezwa kuwa angesajiliwa na mabingwa wa kihistoria kunako ligi kuu.

ISHU YA AJIBU KUFELI TP MAZEMBE YAVUJA KISA BEKI, MABOSI SIMBA WAISHINDWA YANGA

Deprecated: File Theme without comments.php is deprecated since version 3.0.0 with no alternative available. Please include a comments.php template in your theme. in /home/sokalabo/public_html/wp-includes/functions.php on line 6170

Leave a Reply