Uncategorized

MCHUNGAJI MASHIMO, MANARA HAPATOSHI!

admin June 6, 2019 7:15 am


MCHUNGAJI wa Kanisa la Emmaus Bible Church, Daudi Mashimo amemtaka Msemaji wa Timu ya Simba, Haji Manara kumuomba radhi msanii Amber Rutty baada ya kumkashfu mitandaoni.

Hivi karibuni, Mashimo alisema Timu ya Simba haiwezi kuwa bingwa, lakini matokeo yakawa kinyume chake ambapo mapaparazi wachokozi walimuuliza Manara anauchukuliaje utabiri wa mchungaji huyo ndipo akasema;

“Akamtabirie Amber Rutty atapiga tena lini zile ‘picha zake’ na kusambaza mtandaoni.”

Kufuatia kauli hiyo, Mashimo alibuka na kucharuka kwa kusema endapo atagoma kumuomba radhi hadharani atafanya maombi ili msemaji huyo augue tumbo la kuendesha mfululizo mpaka atakapomuomba radhi. “Amuombe radhi Amber Rutty vinginevyo ataona,” alisema Mashimo.

EXCLUSIVE: KAPOMBE ATEMWA RASMI TAIFA STARS ZAHERA ALIAMSHA DUDE YANGA, AWAGOMEA MAKOCHA WAZAWA

Deprecated: File Theme without comments.php is deprecated since version 3.0.0 with no alternative available. Please include a comments.php template in your theme. in /home/sokalabo/public_html/wp-includes/functions.php on line 6170

Leave a Reply