Uncategorized

MOSES KITANDU WA SIMBA, SASA BADO KIDOGO KUTIMKIA KENYA

admin June 9, 2019 11:11 am


STRAIKA wa Simba, Moses Kitandu anayekipiga Coastal Union kwa mkopo yupo mguu nje ndani kutimkia kucheza soka la kulipwa katika timu ya KCB.

Kitandu ambaye KCB walivutiwa na uwezo wake msimu wa mwaka 2017/18 Simba ilipocheza michuano ya SportPesa Cup kwa sasa imeelezwa uongozi wa KCB umerejea tena kuzungumza naye.

Akizungumza na SpotiXtra, Kitandu alisema kuwa kuna mipango mingi ambayo anaifikiria kwa sasa ikiwa ni pamoja na kucheza nje ya nchi.

“Mimi ni mchezaji na ninajua kipaji changu hakifichiki na mpango uliopo kwa sasa ni kucheza nje ya bongo kwa kuwa nimeshatoka Tanga kuna mambo nayafuatilia.

“Siwezi kutaja timu ambayo nakwenda kuitumikia kwani mambo bado hayajakaa sawa nina amini mambo yakikamilika nitataja timu ninayokwenda kuchezea,” alisema Kitandu.

Ni nafasi kwa KMC kuomba kushiriki CECAFA AZAM FC, SIMBA NA YANGA WAGOMBANISHWA NA MSHAMBULIAJI HUYU WA KAGERA SUGAR

Deprecated: File Theme without comments.php is deprecated since version 3.0.0 with no alternative available. Please include a comments.php template in your theme. in /home/sokalabo/public_html/wp-includes/functions.php on line 6170

Leave a Reply