Uncategorized

Kiungo wa Simba amwaga wino Namungo fc

admin June 26, 2019 4:55 am

Kiungo mshambuliaji John Mbise amesajiliwa kwa mkataba wa miaka miwili kutumikia Wana wa Ruhangwa ya Lindi baada ya kuipandisha Ligi Kuu.

John Mbisse aliepitia Simba kati ya mwaka 2014 na 2016 akiwa katika kikosi cha kina Mbaraka Yusuph, Idd Kipagwile, Issa Ngoa na Denis Richard.

Baada ya kumwaga wino John Mbise alisema “Ni furaha kuendelea kubaki Namungo tena, ni wakati mwingine tena wa kuipigania timu ibaki Ligi Kuu kama tulivyoipandisha”

Mchezaji huyo mwenye uwezo wa kucheza nafasi ya kiungo wa kukaba na kushambulia amefunga goli moja huku pia akitoa pasi tatu zaa mabao katika harakati za kuipandisha Namungo fc aliyojiunga nayo dirisha dogo akitokea Friends Rangers.

John Mbise pia amepitia vilabu mbalimbali kama Mshikamano fc, Dodoma fc na Friends Rangers kwa nyakati tofauti.

The post Kiungo wa Simba amwaga wino Namungo fc appeared first on Kandanda.

SIMBA WAONGOZA KIKOSI CHAO KUITWA TWIGA STARS – VIDEO MNYARWANDA WA YANGA ATIMKIA ZAMBIA

Deprecated: File Theme without comments.php is deprecated since version 3.0.0 with no alternative available. Please include a comments.php template in your theme. in /home/sokalabo/public_html/wp-includes/functions.php on line 6170

Leave a Reply