Uncategorized

RUVU SHOOTING YAGOMEA WACHEZAJI WA KIGENI

admin July 3, 2019 11:11 am


UONGOZI wa Ruvu Shooting umesema kuwa kwa sasa hauna mpango wa kusajili wachezaji kutoka nje ya nchi kutokana na kuamini uwezo wa wachezaji wa ndani.

Akizungumza na Saleh Jembe, Ofisa Habari wa Ruvu Shooting, Masau Bwire amesema kuwa  klabu haina hesabu za kusajili nyota wa kigeni.

“Kwenye klabu yetu haitatokea tukasajili wachezaji wa kigeni, sura zao itakuwa ni ngumu kuonekana kwetu kwa kuwa tuna imani na wachezaji wa ndani.

“Kwa sasa tumeanza majaribio ya wachezaji wa ndani tukiwa na lengo la kusuka kikosi kipya hivyo tutawasili kwa kadri watakavyoonyesha uwezo wao,” amesema.

NYOTA WA MBAO FC ATIMKIA KAGERA SUGAR MAALIM BUSUNGU: LIKIJA DILI KUBWA NASAINI

Deprecated: File Theme without comments.php is deprecated since version 3.0.0 with no alternative available. Please include a comments.php template in your theme. in /home/sokalabo/public_html/wp-includes/functions.php on line 6170

Leave a Reply