Home Uncategorized BREAKING: AMUNIKE APIGWA CHINI STARS, MBADALA WAKE AANZA KUSAKWA

BREAKING: AMUNIKE APIGWA CHINI STARS, MBADALA WAKE AANZA KUSAKWA


Inaelezwa kuwa Shirikisho la Soka Tanzania (TFF) limefikia makubaliano ya kuacha na Kocha Emmanuel Amunike aliyekuwa anainoa Taifa Stars.

Hatua hiyo imekuja kufuatia kuboronga mechi za mashindano ya AFCON yanayoendelea Misri.

Taarifa za ndani zinasema TFF hivi sasa ipo kwenye mchakato wa kumpata Mwalimu mbadala wa muda atakayeinoa Stars kuelekea michuano ya CHAN.

SOMA NA HII  KMC KUANZA NA MAJEMBE 11 MAPYA HAYA HAPA