NDEGE ya abiria ya Urusi leo, Agosti 15, 2019, imeanguka baada ya ndege (mnyama) kuingia ndani ya injini na kusababisha mlipuko wa moto katika injini hiyo huko Moscow.
Ndege hiyo ambayo ni Airbus 321 iliyokuwa na abiria 234 pamoja na wahudumu saba ilikuwa ikitoka Urusi kuelekea Simferopol na kulazimika kutua kwa dharura karibu na uwanja wa kimataifa wa Zhukovsky kusini-mashariki mwa Moscow.
Ndege hiyo iliyoangukia katika shamba la mahindi imesababisha Watu 55 kujeruhiwa wakiwemo watoto 17 wenye umri kati ya miaka miwili hadi tisa, ambao wote wapo hospitali kwa matibabu.







