Uncategorized

JAMES KOTEI AZUNGUMZIA ISHU YAKE NA YANGA, KILICHOMKUTA KAIZER CHIEFS ACHA KABISA

admin January 15, 2020 10:57 am


KIUNGO bora ndani ya klabu ya Simba msimu wa mwaka 2018/19 James Kotei ambaye alitimkia Kaizer Chiefs ya Afrika Kusini amekubaliana kuvunja mkataba na klabu hiyo huku akisema kuwa hakuwa na furaha ndani ya timu hiyo.

Kaizer Chief wamefikia hatua hiyo baada ya kumpata mbadala wake kutokana na Kotei kutokuwa na nafasi ndani ya kikosi hicho.

Kotei amesema kuwa alikuwa hapati namba kikosi cha kwanza na hakuwa na furaha ndani ya timu hiyo kutokana na hali hiyo kwani furaha yake ipo kwenye kucheza.

“Sikuwa na furaha kwa kuwa nilikuwa sipati namba, natarajia kupata timu hivi karibuni ila sijazungumza na Yanga jambo lolote kuhusu wao kuhitaji saini yangu,” amesema.

AZAM FC KAZINI TENA EO MBELE YA LIPULI, TAIFA KAGERA SUGAR: MASHABIKI NJOONI MUONE BURUDANI MBELE YA YANGA

Deprecated: File Theme without comments.php is deprecated since version 3.0.0 with no alternative available. Please include a comments.php template in your theme. in /home/sokalabo/public_html/wp-includes/functions.php on line 6170

Leave a Reply