Uncategorized

PONGEZI ZA DHATI KWA WACHEZAJI SIMBA ZATOLEWA

admin January 18, 2020 9:32 pm

Kocha Mkuu wa timu ya Simba SC, Sven Vanderbroeck amewapongeza wachezaji wake baada ya ushindi wa mabao 2-1 dhidi ya Mbao FC katika mchezo wa Ligi Kuu Tanzania Bara kwenye Uwanja wa CCM Kirumba jijinI Mwanza.

Vanderbroeck alisema timu yake ilicheza kwa kupambana sana kuweza kutengeneza nafasi mbili na kuweza kuzitumia vyema. Alisema hali ya hewa ya mvua ilisababisha timu yake ishindwe kucheza mpira wake kutokana na uwanja kutokuwa kwenye hali nzuri.

Alisema Mbao FC walicheza vyema katika nafasi ya kiungo, lakini timu yao ikabadilisha mfumo na kutumia nafasi za winga pamoja na mipira ya kona jambo lilioweza kuwasaidia na kupata ushindi.

Kimsimamo, Simba inaongoza katika msimamo wa ligi hiyo ikiwa na pointi 38 baada ya kushika dimbani mara 15. Kwa upande wake, kocha msaidizi wa timu ya Mbao FC, Abdulmutik Haji alisema timu yake ilicheza vyema licha ya kupoteza mchezo huo.

Alisema timu yake bado ina tatizo katika kutengeneza nafasi za kufunga, hivyo aliahidi wakati wa mazoezi kurekebisha tatizo hilo ili waweze kupata ushindi katika michezo yao ijayo.

Alisema anawaomba wadau na wapenzi wa soka wa timu yao waendelee kuipa sapoti timu yao iweze kufanya vyema katika michezo yao ya Ligi Kuu hidi ya Namungo FC utakaochezwa Februari 3 katika Uwanja wa Majaliwa mkoani Lindi na Februari 6 dhidi ya Ndanda SC huko Nangwanda sijaona mkoani Mtwara.

Katika msimamo wa Ligi Kuu, Mbao FC inayodhaminiwa na Kampuni ya GF Trucks iko katika nafasi ya 14 baada ya kujikusanyia pointi 18 kutokana na
mechi 17 ilizocheza hadi sasa.
UKIACHANA NA SOKA, HIKI NI KIPAJI KINGINE CHA DAVID MOLINGA ‘FALCAO’ YANGA BHANA, KAMA MLIVYOSIKIA!! SPOTI XTRA KATIKA UKURASA WA MBELE LEO JUMAPILI

Deprecated: File Theme without comments.php is deprecated since version 3.0.0 with no alternative available. Please include a comments.php template in your theme. in /home/sokalabo/public_html/wp-includes/functions.php on line 6170

Leave a Reply