Uncategorized

SADIO MANE NI BALAA TUPU NDANI YA LIGI KUU ENGLAND

admin February 17, 2020 4:22 am

SADIO Mane, nyota wa timu ya Liverpool amefikisha jumla ya mabao 100 ndani ya Ligi Kuu ya England.

Mane alifikisha bao hilo kwenye mechi dhidi ya Norwich alipopachika bao 1 la ushindi na kuipa pointi tatu timu yake.

 Bao hilo alifunga akitokea benchi na kuwafanya wafikishe jumla ya pointi 76 kwenye ligi wakiwa nafasi ya kwanza na mabingwa watetezi Manchester City wapo nafasi ya pili wakiachwa kwa jumla ya pointi 25.

Endapo Liverpool itashinda mechi zake tano zinazofuata ndani ya ligi kati ya 13 watatangazwa kuwa mabingwa bila kujali matokeo ya timu nyingine.

MUONEKANO WA UKURASA WA MBELE GAZETI LA CHAMPIONI JUMATATU AZAM FC:LIGI NGUMU KWELI

Deprecated: File Theme without comments.php is deprecated since version 3.0.0 with no alternative available. Please include a comments.php template in your theme. in /home/sokalabo/public_html/wp-includes/functions.php on line 6170

Leave a Reply