Uncategorized

SIMBA YAWEKA REKODI HII BONGO, YAIACHA YANGA KWA POINTI 21

admin February 24, 2020 10:11 am


SIMBA imeweka rekodi yake ndani ya Ligi Kuu Bara kwa  kuwa ni timu yenye mabao mengi kuliko zote kwa sasa huku ikiwapoteza kwa mbali watani zao wa jadi Yanga.

Simba imefunga mabao 50 kwenye mechi zake 24 ambazo imecheza huku ikiongoza ligi na pointi zake 62.

Watani wao wa jadi Yanga wameachwa nyuma licha ya kuwa na mechi mbili mkononi kwani Yanga imecheza mechi 22 imefunga mabao 25 na ina pointi 41 kibindoni.

Ina deni la pointi 21 ili kuweka mzani sawa huku kwenye upande wa mabao ikidaiwa mabao 25 ili kuweka usawa na Simba yenya mabao 50.

Singida United iliyo nafasi ya 19 ndiyo inayofunga kwenye hesabu za timu zenye mabao machache imecheza mechi 24 na imefunga mabao 13 ikiwa imejikusanyia pointi12.

Kinara wa utupiaji kwa Simba ni Meddie Kagere mwenye mabao 14 na kwa Yanga ni David Molinga mwenye mabao saba.

HII HAPA RATIBA YA KOMBE LA SHIRIKISHO HIZI HAPA DAKIKA 180 ZA MOTO KWA YANGA NA SIMBA KABLA YA MACHI 8

Deprecated: File Theme without comments.php is deprecated since version 3.0.0 with no alternative available. Please include a comments.php template in your theme. in /home/sokalabo/public_html/wp-includes/functions.php on line 6170

Leave a Reply