Uncategorized

CHAN NA AFCON KUPANGIWA TAREHE, KAMBI YA STARS YAVUNJWA

admin March 18, 2020 2:42 pm


MASHINDANO ya CHAN ambayo yanawashirikisha wachezaji wa ligi za ndani pamoja na yale ya Afcon yatapagiwa tarehe kulingana na hali itakavyokuwa ya ugonjwa wa Corona.

Dunia kwa sasa inapambana kutafuta kinga na dawa za virusi vya Corona ambavyo vimeanza kusambaa mwezi Januari nchini China.

 CAF imesitisha mashindano ya CHAN yaliyokua yafanyike Cameroon kuanzia Aprili 4-25,2020 mpaka pale hali ya ugonjwa wa Corona itakapotulia pia hata Afcon pia ilipaswa ifanyike nchini humo.

Taarifa ya CAF inasema imechukua hatua hiyo ili kulinda afya za Wachezaji,Viongozi,washirika na mashabiki. 


Timu ya Taifa ya Tanzania iliyo chini ya Etienne Ndayiragije ambayo ilikuwa imeweka kambi kwa ajili ya maandalizi ya CHAN nayo imevunjwa.

MPANGO MKUBWA WA KUMALIZA LIGI KUU ENGLAND UPO NAMNA HII SASA LIGI KUU BARA KUCHEZWA BILA MASHABIKI UWANJANI

Deprecated: File Theme without comments.php is deprecated since version 3.0.0 with no alternative available. Please include a comments.php template in your theme. in /home/sokalabo/public_html/wp-includes/functions.php on line 6170

Leave a Reply