Uncategorized

SASA LIGI KUU BARA KUCHEZWA BILA MASHABIKI UWANJANI

admin March 18, 2020 2:42 pm


KIKAO cha Kamati ya Uongozi cha TFF kimeazimia kuwa, baada ya siku 30 Serikali itakaporuhusu michezo kuendelea, mechi za Ligi Kuu Bara, Ligi Daraja la Kwanza, Ligi Daraja la Pili na Ligi ya Mabingwa wa Mikoa (RCL) zitachezwa bila watazamaji, ili kudhibiti kusambaa kwa virusi vya Corona.

Taarifa hiyo imetolewa leo na Mtendaji Mkuu wa Bodi ya Ligi, Almas Kasongo mara baada ya kikao hicho ambacho kimehudhuriwa pia na Rais wa TFF, Wallace Karia.

Kasongo amesema pia kuwa wachezaji wote watafanyiwa vipimo maalum kuchunguzwa endapo wameathirika na virusi vya Corona au la kabla ya ligi hizo kurejea.


Serikali kupitia kwa Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa, jana Machi 17 ilisitisha mwendelezo wa masuala yote ya michezo na mikusanyiko isiyo ya lazima ili kupambana na kasi ya kusambaa kwa Virusi vya Corona.

CHAN NA AFCON KUPANGIWA TAREHE, KAMBI YA STARS YAVUNJWA YANGA: TULIWABANA MBAVU NAMUNGO, WASHUKURU MWAMUZI

Deprecated: File Theme without comments.php is deprecated since version 3.0.0 with no alternative available. Please include a comments.php template in your theme. in /home/sokalabo/public_html/wp-includes/functions.php on line 6170

Leave a Reply