Uncategorized

NYOTA WA CHELSEA APEWA RUHUSA KUIONA FAMILIA YAKE

admin March 26, 2020 6:52 pm


TIMU ya Chelsea imekubali kumpa ruhusa nyota wake Willian Borges Da Silva kurejea kuiona familia yake.

Winga huyo raia wa Brazil aliomba ruhusa ya kurejea kwao ili kuiona familia yake wakati huu wa tatizo la Virusi vya Corona.

Chelsea iliyopo London imekubali kumpa ruhusa winga huyo akamuone mkewe na wanae ambao wapo Brazil.

Kwa sasa Ligi Kuu England imesimamishwa kwa muda na inatarajia kurejea Aprili 30 endapo hali ya maambukizi itapungua na kutulia.

Nyota huyo amedumu ndani ya Stamford Bridge kwa muda wa miaka saba na mkataba wake unameguka Juni huku hatma yake kubaki ndani ya klabu hiyo kwani Cheksea ilitaka kumpa kandarasi ya mwaka mmoja yeye alitaka apewe ya miaka miwili.

KANE:NIPO FITI NITAREJEA UWANJANI HIVI KARIBUNI AKILI ZA HARUNA NIYONZIMA NDANI YA CHAMPIONI IJUMAA

Deprecated: File Theme without comments.php is deprecated since version 3.0.0 with no alternative available. Please include a comments.php template in your theme. in /home/sokalabo/public_html/wp-includes/functions.php on line 6170

Leave a Reply