Uncategorized

NONGA: UBORA WA WACHEZAJI WENZANGU UNANIFANYA NAKUWA BORA

admin March 31, 2020 3:51 am

PAUL Nonga, nahodha wa Lipuli amesema kuwa kinachomfanya kuwa bora ndani ya Lipuli ni kutokana na ubora wa wachezaji anaocheza nao.

Nonga ni miongoni mwa manahodha wazawa wenye mabao mengi ndani ya Ligi Kuu Bara akiwa amefunga mabao 11 nahodha mwingine mwenye mabao sawa na Nonga ni Reliants Lusajo anayekipiga Namungo.

Akizungumza na Saleh Jembe, Nonga amesema kuwa kinachombeba ndani ya Lipuli ni pamoja na ubora wa wachezaji ambao anacheza nao kwa kuelewana na kupeana majukumu.

“Aina ya wachezaji ambao ninacheza nao pamoja na namna ambavyo kila mmoja anapokea majukumu aliyopewa ni vitu muhimu kuzingatia kwani vinaongeza ubora,” amesema.

MBELGIJI WA SIMBA ATAJA KINACHOWAWEKA BENCHI AJIBU, MLIPILI,NDEMLA NYOTA WA KMC ATAJA SABABU ZA MEDDIE KAGERE KUFUNGA MABAO

Deprecated: File Theme without comments.php is deprecated since version 3.0.0 with no alternative available. Please include a comments.php template in your theme. in /home/sokalabo/public_html/wp-includes/functions.php on line 6170

Leave a Reply