Uncategorized
YANGA WAMEAMUA, SASA KUMVUTIA KASI KIUNGO HUYU MATATA ANAYEKIPIGA TIMU YA TAIFA
IMEELEZWA kuwa Klabu ya Yanga inaisaka saini ya nyota wa Kariobangi Sharks FC Yidah Sven Yidah ili aongeze nguvu kwenye kikosi hicho.
Nyota huyo ambaye ni kiungo raia wa Kenya anakipiga pia kwenye timu ya Taifa ya chini ya miaka 23.
Uwezo wake wa kukaba na kuzuia mashambulizi ya wapinzani inaelezwa kuwa sababu ya Yanga kuvutiwa naye na ikiwa mambo yatakwenda sawa anaweza kutua bure kwani mkataba wake unameguka mwisho wa msimu huu.
Ofisa Uhamasishaji wa Yanga, Antonion Nugaz amesema kuwa kwa sasa ni subira inahitajika kwani mpango mkubwa uliopo ni kusuka kikosi kipya.
Leave a Reply
You must be logged in to post a comment.