Uncategorized

KOCHA SIMBA AMPA MAKAVU CHILUNDA WA AZAM FC

admin May 9, 2020 8:40 am

JAMHURI Kihwelo ‘Julio’, kocha wa zamani wa Simba amesema kuwa mchezaji wa Azam FC, Shabani Idd Chilunda, ni mfano mzuri wa wachezaji wengi wa Kibongo wenye vipaji vya hali ya juu lakini hawajitumi.
Akizungumzia suala la wachezaji wengi wa Kibongo kushindwa kufanya vizuri nje ya nchi, Julio alisema:-“Unajua Tanzania kuna wachezaji wengi wenye vipaji ila hawajitumi, ndiyo maana tunashindwa kuwa na wachezaji wengi wanaocheza soka la kulipwa nje ya nchi.
“Mfano mzuri ni Chilunda ambaye unaweza kuona kipaji kikubwa alichonacho lakini amekuwa hajitumi kama ambavyo inatakiwa, ndiyo maana anaweza kutamba hapa nchini lakini alishindwa maisha ya nchini Hispania.
“Na hili ndiyo tatizo kubwa la wachezaji wetu, nakumbuka mimi wakati naifundisha Simba tulikuwa tunagombana sana na wachezaji wengi kwa sababu wanataka kusukumwa hadi kwenye suala la mazoezi,” alisema Julio.

Chanzo: Championi
HASSAN DILUNGA AANZA KUAGA SIMBA ARGUERO NI CHUMA CHA MABAO NDANI YA CITY

Deprecated: File Theme without comments.php is deprecated since version 3.0.0 with no alternative available. Please include a comments.php template in your theme. in /home/sokalabo/public_html/wp-includes/functions.php on line 6170

Leave a Reply