Uncategorized

SONSO YUPO TAYARI KWA MAPAMBANO NDANI YA LIGI KUU BARA

admin May 25, 2020 4:47 am

BEKI wa Yanga, Ally Mtoni ‘Sonso’ amesema kuwa yupo tayari kwa ajili ya mapambano ndani ya Ligi Kuu Bara kumaliza mechi zilizosalia ndani ya msimu wa 2019/20.

Masuala ya michezo yalisimamishwa na Serikali, Machi 17 kutokana na janga la Virusi vya Corona na inatarajiwa kurejea Juni Mosi baada ya Serikali kusema kuwa hali imeanza kuwa shwari.

Sonso amesema kuwa wakati wa mapumziko ya lazima alikuwa anafanya mazoezi binafsi hivyo anaamini bado anaweza kuhimili mikiki ya ndani ya Uwanja.

 “Nilikuwa ninafanya mazoezi binafsi hivyo hainipi tabu kurejea kwenye mechi za ushindani imani yangu kwamba nitafanya vizuri na kwa kushirikiana na wenzangu tutapata matokeo chanya. 

“Kikubwa sapoti na kusubiri kuona mambo yatakavyokuwa kukaa bila kucheza tulikuwa tumekumbuka mpira,” amesema.

GSM KIBOKO YAMPA MKATABA NYOTA HUYU,NDANI YA CHAMPIONI JUMATATU HAPA NDIPO ALIPO MBWANA SAMATTA

Deprecated: File Theme without comments.php is deprecated since version 3.0.0 with no alternative available. Please include a comments.php template in your theme. in /home/sokalabo/public_html/wp-includes/functions.php on line 6260

Leave a Reply