Uncategorized

BEKI WA NKANA FC, HASSAN KESSY ATAJA ATAKAPOKUWA IWAPO DILI LAKE LITABUMA NKANA

admin May 30, 2020 9:47 pm


HASSAN Kessy, beki wa Nkana FC inayoshiriki Ligi Kuu ya nchini Zambia amesema kuwa akikwama kubaki ndani ya klabu hiyo ataibukia Afrika Kusini.

Mkataba wa Kessy ndani ya Nkana FC unameguka mwishoni mwa msimu huu na mpaka sasa hakuna mazungumzo yoyote na mabosi wake kutokana na shughuli za michezo kusimamishwa kutokana na janga la Virusi vya Corona.


Nyota huyo amesema kuwa hesabu zake ni kusonga mbele zaidi ya hapo alipo kwa sasa na anafikiria kwenda Afrika Kusini. 


“Nawaza kwenda kucheza mbele sio kurudi nyuma kwani kwa sasa mkataba wangu na Nkana unakaribia kuisha na hakuna mazungumzo ya kuongeza mkataba kwa kuwa michezo kule haijulikani itarejea lini,” .

HUYU HAPA NI MBABE WA SARE, YANGA NA SIMBA WANAJUA SHUGHULI YAKE HII HAPA MITAMBO MINGINE YA MABAO NDANI YA SIMBA

Deprecated: File Theme without comments.php is deprecated since version 3.0.0 with no alternative available. Please include a comments.php template in your theme. in /home/sokalabo/public_html/wp-includes/functions.php on line 6260

Leave a Reply