Uncategorized

MTIBWA SUGAR: TUPO TAYARI KWA AJILI YA KUENDELEA KUPAMBANA

admin May 28, 2020 12:47 pm

THOBIAS Kifaru, Ofisa Habari wa Mtibwa Sugar amesema kuwa wapo tayari kwa ajili ya ushindani kutokana na wachezaji wao kuwa na mwendelezo wa mazoezi wakati wa mapumziko yaliyosababishwa na Virusi vya Corona.
Akizungumza na Saleh Jembe,Kifaru amesema kuwa wapo tayari kwa ushindani wakati wowote kutokana na uimara wa falsafa yao na wachezaji makini walionao.
” Tupo tayari kwa ajili ya ligi na kila kitu kipo vizuri kwa sasa ni kufanya maandalizi ya mwisho kabla ya vijana kurudi uwanjani kwani wakati wa mapumziko yaliyosababishwa na janga la Corona vijana walikuwa wanafanya mazoezi.
“Kikubwa ni kuendelea kuchukua tahadhari dhidi ya Corona kwani bado janga lipo nasi tutaendelea kuchukua tahadhari ili tuwe salama,” amesema.
Tayari Mtibwa Sugar wameanza mazoezi kwa ajili ya kujiweka sawa ili ligi itakaporejea mambo yaende vizuri.
MIKONO YA DHAHABU YA ABAROLA YAPOTEZWA NA MANULA SVEN ACHEKELEA KUREJEA KWA SHEVA

Deprecated: File Theme without comments.php is deprecated since version 3.0.0 with no alternative available. Please include a comments.php template in your theme. in /home/sokalabo/public_html/wp-includes/functions.php on line 6170

Leave a Reply