Uncategorized

OLE GUNNAR APANGA KUMTUMIA POGBA NA BRUNO

admin June 10, 2020 5:47 am


OLE Gunnar Solskjaer, Kocha Mkuu wa Manchester United inaripotiwa kuwa amepanga kumtumia kiungo wake Paul Pogba kucheza namba 10 sambamba na kiungo Bruno Fernandes.

Pogba tayari amesharejea kutoka kutibu majeraha yake ya enka ambayo aliyapata jambo ambalo linampa matumaini makubwa Solsksjaer kuona namna atakavyokuwa na kikosi kipana chenye muunganiko makini.

Tayari Pogba ameanza mazoezi na wachezaji wenzake huku akiwa ni mwenye furaha na aliweza kuonana na kiungo mwenzake Fernades ambaye amekuwa na msaada mkubwa ndani ya kikosi cha United.

Kiungo huyo hajacheza mechi ya ushindani tangu Boxing day mwaka jana kutokana na kutumia muda mwingi kutibu majeraha yake.
RAIS LA LIGA AELEZA MTAZAMO WAKE KUHUSU USHIRIKIANO NA YANGA MBELGIJI WA YANGA KUTUA LEO

Deprecated: File Theme without comments.php is deprecated since version 3.0.0 with no alternative available. Please include a comments.php template in your theme. in /home/sokalabo/public_html/wp-includes/functions.php on line 6260

Leave a Reply