Uncategorized

BERNARD MORRISON AONGEZA IDADI YA WATAKAOUKOSA MCHEZO WA MWADUI FC

admin June 12, 2020 11:47 am


BERNARD Morrison, anaongeza orodha ya wachezaji wa Yanga watakaoukosa mchezo wa kesho dhidi ya Mwadui FC.

Wengine ambao wataukosa mchezo huo ni pamoja na Papy Tshishimbi ambaye ni nahodha kwa mujibu wa Ofisa Habari wa Yanga, Hassan Bumbuli amesema kuwa bado hajawa fiti.

Ally Ally na Erick Kabamba, hawapo kwenye mpango wa sasa mpaka mchezo ujao.

Habari zinaeleza kuwa Morrison ilipaswa kwenda na Kocha leo Shinyanga ila imeshindikana kutokana na sababu ambazo hazijawekwa wazi.

“Morrison alipaswa kuondoka leo na Kocha Mkuu, Luc Eymael ila imeshindikana ndio maana ameondoka David Molinga kwenda kuchukua nafasi yake,” ilieleza taarifa hiyo.

Juni 14 Yanga itamenyana na Mwadui FC, Uwanja wa Kambarage.

WAWA AIPIGA MKWARA MZITO AZAM FC SIMBA YATOA TAMKO KUHUSU MOLINGA, YAICHOKONOA YANGA KIMTINDO

Deprecated: File Theme without comments.php is deprecated since version 3.0.0 with no alternative available. Please include a comments.php template in your theme. in /home/sokalabo/public_html/wp-includes/functions.php on line 6170

Leave a Reply