Uncategorized

BREAKING:MORRISON WA YANGA ASAINI SIMBA

admin August 8, 2020 11:47 am

 

BREAKING:BERNARD Morrison kiungo mshambuliaji wa Yanga leo ametambulishwa ndani ya kikosi cha Simba.


Morrison mwenye mabao manne ndani ya Ligi Kuu Bara wakati akikipiga Yanga alikuwa kwenye mvutano mkubwa na mabosi wake kwenye suala la mkataba ambapo mchezaji alisema kuwa ana dili la miezi sita huku uongozi ukisema kuwa amesaini dili la miaka miwili.

Leo Agosti 8, Morrison amevalishwa uzi mwekundu na kuonekana akisaini dili jipya la kujiunga na Simba.

Huu unakuwa usajili wa kwanza kwa Simba kutambulishwa rasmi kwa ajili ya msimu wa 2020/21.

Thamani ya dau lake inatajwa kuwa ni zaidi ya milioni 150 ambayo amepewa ili kujiunga na klabu ya Simba huku akitajwa kupewa dili la miaka miwili.




SAMAKIBA LEO HAPATOSHI, MORRISON HATIHATI KUKOSA TIMU KWA MKAPA MRISHO NGASSA WA YANGA ANUKIA GWAMBINA FC

Deprecated: File Theme without comments.php is deprecated since version 3.0.0 with no alternative available. Please include a comments.php template in your theme. in /home/sokalabo/public_html/wp-includes/functions.php on line 6170

Leave a Reply