Uncategorized

MANCHESTER CITY KUTOA WACHEZAJI WATATU KUMPATA MESSI

admin August 30, 2020 11:47 am

 


MAN City imeripotiwa kuwa ipo tayari kuipa Barcelona pauni milioni 89.5 pamoja na wachezaji watatu; Bernardo Silva, Gabriel Jesus na Eric Garcia ili kumpata supastaa Lionel Messi.

 

City wanamatumaini makubwa ya kufikia makubaliano na Barcelona baada ya Messi kutangaza hivi karibuni juu ya nia yake ya kuondoka Camp Nou katika kipindi hiki cha usajili.

 

Kama Messi akikubaliana na City, ataungana tena na kocha wake wa zamani Pep Guardiola baada ya miaka yake ya mafanikio Nou Camp akifunga mabao 634 na kutoa asisti 285 kwenye mechi 731 alizoicheza.



Sportsmail inaelewa kuwa Messi na Guardiola wamekuwa wakiwasiliana kupitia simu juu ya kutua kwake Etihad, hata kujadili jinsi Messi atakavyozoea England na kujifunza Kiingereza baada ya miaka 20 Hispania.

 

Wazo la kumsajili Messi kwa muda mrefu lilionekana kama ndoto isiyowezekana lakini dau la pauni milioni 89.5 kujumlisha Silva, Jesus na Garcia linaweza kufanya usajili huo utimie.

JEMBE LA KAZI YANGA LAANZA SAFARI KUJA BONGO KIKOSI CHA SIMBA KITAKACHOANZA LEO DHIDI YA NAMUNGO FC NGAO YA JAMII

Deprecated: File Theme without comments.php is deprecated since version 3.0.0 with no alternative available. Please include a comments.php template in your theme. in /home/sokalabo/public_html/wp-includes/functions.php on line 6260

Leave a Reply