Uncategorized

KOCHA YANGA ABEBA MATUMAINI TIMU YAKE KUFANYA VIZURI

admin September 10, 2020 5:47 am


 KOCHA Mkuu wa Yanga, Zlatko Krmpotic amesema kuwa anaamini uwezo wa wachezaji wake unazidi kuimarika kila siku jambo linalompa matumaini ya kufaya vizuri kwenye mechi zake zijazo.

Zlatko amesema kuwa kwa namna wachezaji wake wanavyocheza wana kitu cha kipekee ambacho kinampa matumaini ya kuweza kufanya vema kwenye mechi zake zinazofuata.

“Kwa namna ambavyo wachezaji wanacheza kuna kitu cha kipekee ambacho kipo kwao, imani yangu ni kwamba baada ya muda watakuwa tayari kutoa kilicho bora kwa kuwa kwa sasa wanashindwa kwa kuwa bado hawajawa na muunganiko mzuri.


“Mwanzo wa sare sio mbaya kwani nimeona namna ambavyo wachezaji walikuwa wakicheza kwa kuwa ni mchezo wa kwanza huwezi kulaumu, kinachofuata kwa sasa ni kuendelea kujipanga kwa ajili ya mechi zinazofuata,” amesema.

Yanga Septemba 13 ina kibarua kingine cha kumenyana na  Mbeya City iliyopoteza kwa kufungwa mabao 4-0 na KMC, Uwanja wa Mkapa.Septemba 7.
MAJEMBE HAYA MATANO YA KAZI SIMBA, KAMILI GADO KUIVAA MTIBWA SUGAR KIUNGO MPYA SIMBA MZAMBIA ANAWAZA MATAJI TU

Deprecated: File Theme without comments.php is deprecated since version 3.0.0 with no alternative available. Please include a comments.php template in your theme. in /home/sokalabo/public_html/wp-includes/functions.php on line 6170

Leave a Reply