Uncategorized

KUPOTEZA MBELE YA SPURS, LAMPARD HATA HAELEWI

admin September 30, 2020 5:47 am


 FRANK Lampard, Kocha Mkuu wa Chelsea amesema kuwa kupoteza kwake mbele ya Tottenham Hotspurs kumemvuruga kwa kuwa walianza kushinda ndani ya dakika 45 za mwanzo.

Mchezo huo wa Kombe la Carabao hatua ya 16 bora uliochezwa usiku wa kuamkia leo, Uwanja wa Tottenham Hotspur ulikuwa na ushindani mkubwa na dakika 90 zilikamilika kwa sare ya kufungana bao 1-1 jambo lililopelekea mshindi kupatikana kwa penalti.

Timo Werner dakika ya 19 alianza kufunga kwa Chelsea na lilisawazishwa dakika ya 83 na Erik Lamela ambapo kwenye penalti, Spurs inayonolewa na Jose Mourinho ilishinda penalti 5-4.Mason Mount alikosa penalti kwa upande wa Chelsea.

Lampard amesema kuwa wachezaji wake walionekana wamechoka kwenye mchezo huo jambo lililowafanya washindwe kuibuka na ushindi jumlajumla.

“Tulikiwa tunahitaji kubaki kwenye ushindani ila inaonekana wachezaji wangu walikuwa wamechoka,kwa hali ile ilikuwa ngumu kupata matokeo chanya na ilikuwa ni ngumu kwetu kupoteza kwa kuwa tulianza kushinda,” amesema.

PRINCE DUBE WA AZAM FC ALA SAHANI MOJA NA MEDDIE KAGERE WA SIMBA MWINYI ZAHERA: SIMBA INA KIKOSI BORA MSIMU WA 2020/21

Deprecated: File Theme without comments.php is deprecated since version 3.0.0 with no alternative available. Please include a comments.php template in your theme. in /home/sokalabo/public_html/wp-includes/functions.php on line 6170

Leave a Reply