Uncategorized

MARCEL KAHEZA AFICHUA KILICHO NYUMA YA MAFANIKIO

admin September 30, 2020 10:47 am


 MARCEL Kaheza mshambuliaji namba moja ndani ya kikosi cha Polisi Tanzania amesema kuwa kikubwa kinachoipa ushindi timu yake ni ushirikiano ambao wanauonyesha wachezaji wakiwa uwanjani pamoja na mbinu za mwalimu.


Polisi Tanzania inafundisha na Malale Hamsini ambaye ni Kocha Mkuu, mchezo wake uliopita wa raundi ya nne ilishinda mabao 3-0 mbele ya Dodoma Jiji mchezo uliochezwa Uwanja wa Jamhuri, Dodoma.

Kaheza anashikilia rekodi ya kufunga mabao mengi kwenye raundi ya nne ambapo alifunga mabao mawili kwenye ushindi wa mabao 3-0 mbele ya Dodoma Jiji.

Nyota huyo amesema:”Mwalimu amekuwa akitupa mbinu nyingi kwa ajili ya kutafuta ushindi nasi pia tumekuwa tukizifuata, sapoti kutoka kwa mashabiki na ushirikiano ambao tunaupata ni jambo ambalo linatupa ushindi.”


Mchezo wao unaofuata kwa Polisi Tanzania ni Oktoba 5, Uwanja wa Uhuru itakuwa dhidi ya KMC ambayo imetoka kupoteza kwa kufungwa bao 1-0 mbele ya Kagera Sugar.

AZAM FC YAANZA KUJIWEKA MGUU SAWA KWA AJILI YA KUMENYANA NA KAGERA SUGAR MITAMBO HII YA MABAO NDANI YA SIMBA YAMPA JEURI SVEN

Deprecated: File Theme without comments.php is deprecated since version 3.0.0 with no alternative available. Please include a comments.php template in your theme. in /home/sokalabo/public_html/wp-includes/functions.php on line 6170

Leave a Reply