Uncategorized

KAZE ASAINI DILI LA MIAKA MIWILI YANGA

admin October 16, 2020 10:47 am


 UONGOZI wa Klabu  ya Yanga leo Oktoba 16 umemtambulisha rasmi Kocha Mkuu Cedric Kaze, ambaye amesaini mkataba wa miaka miwili kuwa ndani ya klabu hiyo.


Kaze alitua Bongo usiku wa kuamkia leo akitokea nchini Canada na kupokelewa na viongozi wa Yanga pamoja na mashabiki.

Amekuja kuchukua mikoba ya Zlatko Krmpotic ambaye alifutwa kazi Oktoba 3 kutokana na kile kilichoelezwa kuwa hakuwa na mwendo mzuri ndani ya kikosi hicho.

Raia huyo wa Burundi amesema kuwa anafurahi kuwa ndani ya kikosi cha Yanga kwa kuwa anakitambua na anahitaji ushirikiano.

Mkataba huo utamfanya awatumikie Wananchi hadi 2020/22.
RATIBA YA VPL LEO NI JAMHURI, DODOMA SIMBA YAZUNGUMZIA POINTI ZA YANGA

Deprecated: File Theme without comments.php is deprecated since version 3.0.0 with no alternative available. Please include a comments.php template in your theme. in /home/sokalabo/public_html/wp-includes/functions.php on line 6260

Leave a Reply