Uncategorized

POGBA: NILIFANYA KOSA LA KIJINGA NDANI YA UWANJA

admin November 2, 2020 10:47 am


 KIUNGO wa kati wa Manchester United, Paul Pogba, amekubali kupokea lawama baada ya kucheza rafu dhidi ya mchezaji wa Arsenal, iliyosababisha penati ambayo iliamua matokeo ya mchezo huo wa ligi kuu ya England.

 

Pogba alinyanyua mguu uliomuangusha Hector Bellerin ndani ya eneo la hatari na Pierre-Emerick Aubameyang akafunga bao lililoipa ushindi Uwanja wa Old Trafford.

 

”Tunajua kwamba kilikuwa ni kiwango duni, mimi binafsi sikupaswa kucheza rafu ya aina ile. Nilidhani ningeugusa mpira lakini sikufanya hivyo. Sikupaswa kutoa adhabu mbaya kama hiyo.




“Nilicheza faulo ya kijinga na nimefanya kosa la kijinga ambalo limeigharimu timu yangu, nimefanya makosa ila hamna namna kwa kuwa nilikuwa ninapambana kutimiza majukumu yangu,” amesema Pogba.


LUSAJO NYOTA WA KMC ALIYEIBUKIA KUTOKA NAMUNGO ATAJA MABAO ATAKAYOFUNGA VIGONGO VITANO VYA MOTO KWA SIMBA ACHA KABISA, YANGA NDANI

Deprecated: File Theme without comments.php is deprecated since version 3.0.0 with no alternative available. Please include a comments.php template in your theme. in /home/sokalabo/public_html/wp-includes/functions.php on line 6260

Leave a Reply