Uncategorized

MITAMBO YA MABAO YA SIMBA YAREJEA KIKOSINI

admin November 23, 2020 2:47 am

 


MITAMBO ya mabao ndani ya Klabu ya Simba, Meddie Kagere na Luis Miquissone imerejea na kuanza mazoezi pamoja na wachezaji wengine ndani ya kikosi hicho.


Nyota hao wawili hawakuwa sehemu ya kikosi kilichoibuka na ushindi wa mabao 0-7 dhidi ya Coastal Union ya Tanga kwenye mchezo wa Ligi Kuu Bara uliochezwa Uwanja wa Sheikh Amri Abeid. 


Luis raia wa Msumbiji na Kagere wa Rwanda walichelewa kujiunga na wachezaji wenzao kwa kuwa walikuwa Kwenye majukumu ya timu zao za Taifa katika harakati za kuwania tiketi ya kufuzu Afcon. 


Simba ikiwa imefunga mabao 29, wawili hawa wamehusika Kwenye mabao 11,Kagere ametupia mabao manne na Luis amefunga bao moja na kutoa pasi sita za mabao.

MSIMAMO WA LIGI KUU TANZANIA BARA HESABU ZA SIMBA NI KWA WANIGERIA, SVEN ATOA NENO

Deprecated: File Theme without comments.php is deprecated since version 3.0.0 with no alternative available. Please include a comments.php template in your theme. in /home/sokalabo/public_html/wp-includes/functions.php on line 6170

Leave a Reply