Uncategorized

COASTAL WASEPA NA POINTI TATU ZA IHEFU, MABAO 7 YA SIMBA YANAWATESA

admin November 24, 2020 7:47 pm


 JUMA Mgunda, Kocha Mkuu wa Coastal Union amesema kuwa mabao 7-0 waliyopata mbele ya ya Simba bado yapo kwenye vichwa vyao jambo ambalo linamfanya apate muda wa kukaa nao ili waweze kufanya vizuri kwenye mechi zao zijazo.


Bao pekee la Coastal Union lilipachikwa kimiani na nahodha Salum Ally dakika 16 akiwa nje ya 18 kwa guu lake la kulia lililomshinda mlinda mlango namba moja wa Ihefu, Isihaka Joseph.

Mchezo wa Ihefu uliopita walilazimisha sare ya bila kufungana na Polisi Tanzania, Uwanja wa Azam Complex na leo wamekubali kupoteza kwa kufungwa bao 1-0 Uwanja wa Mkwakwani, Tanga.

Mgunda amesema:”Vijana wamepambana kwa kadri ya uwezo ila naona kwamba licha ya kupata ushindi bado wanashindwa kurekebisha makosa yao, yale makosa yao yanajirudiarudia hasa ya mchezo uliopita.


“Ambacho nitakifanya ni kukaa nao chini kuzungumza ili kuweza kutoa makosa yale yaliyopita ili kuona namna gani tutaweza kuwa bora, bado nafasi ipo na tunaamini tutafanya vizuri,” .

MUGALU YAMKUTA KWA SVEN, KAZE ANA JAMBO LAKE SIMBA YATUA ETHIOPIA, KUWAFUATA WAPINZANI WAO KIMATAIFA KESHO

Deprecated: File Theme without comments.php is deprecated since version 3.0.0 with no alternative available. Please include a comments.php template in your theme. in /home/sokalabo/public_html/wp-includes/functions.php on line 6170

Leave a Reply