Uncategorized

NYOTA KMC ASIMAMISHWA KISA NIDHAMU

admin January 7, 2021 9:47 am


UONGOZI wa 
Klabu ya KMC FC umemsimamisha mshambuliaji wa kikosi hicho Relliants Lusajo aliyeibuka ndani ya kikosi hicho akitokea Klabu ya Namungo. 


Taarifa iliyotolewa na Ofisa Habari wa KMC,Christian Mwagala imeeleza namna hii:”Tunapenda kuwajulisha mashabiki na wapenzi wa Klabu ya KMC FC kuwa mchezaji Realint Lusajo amesimamishwa kutokana na sababu ya utovu wa nidhamu.


“Uamuzi huo umefikiwa ikiwa ni baada ya uongozi kujiridhisha na kwamba mchezaji yoyote anapofanya makosa ya utovu wa nidhamu kwenye Timu atapaswa kupata adhabu ikiwa ni pamoja na kusimamishwa.


“Wakati huo huo,uongozi wa KMC FC pia umetoa mapumziko ya siku 10 kwa wachezaji wake na kwamba watapaswa kurejea kambini Januari 15 mwaka huu kwa ajili ya kuanza maandalizi ya michezo ya Ligi kuu Soka ,”Tanzania Bara ambapo mchezo unaofuata KMC FC watakuwa ugenini dhidi ya Tanzania Prisons.


MSIMAMO WA LIGI KUU TANZANIA BARA UPO NAMNA HII 2021 UWE WA KIPEKEE KWA WAWAKILISHI WETU KIMATAIFA

Deprecated: File Theme without comments.php is deprecated since version 3.0.0 with no alternative available. Please include a comments.php template in your theme. in /home/sokalabo/public_html/wp-includes/functions.php on line 6170

Leave a Reply