Uncategorized

WACHEZAJI KUPIMWA CORONA MARA MBILI KWA WIKI

admin January 12, 2021 7:47 am


TIMU zote 20 zinazoshiriki Ligi Kuu England kwa sasa wachezaji pamoja na viongozi watalazimika kupima Virusi ya Corona mara mbili ndani ya wiki moja ili kuendelea kukabiliana na maambukizi mapya ya Corona.

Hali hii imekuja kutokana na maambukizi ya Corona kuzidi kuwa na kasi ambapo hivi karibuni iliripotiwa visa jumla ya 36 kwa waliopimwa ikijumuisha wachezaji pamoja na viongozi ndani ya timu shiriki.

Imeripotiwa kuwa ndani ya mwezi Januari jumla ya vipimo 2,593 kati ya Januari 4 na 10 vilifanyika  na maambukizi yameonekana kuwa kwa asilimia 1.39 kwa waliopimwa.

Mpaka sasa kutokana na janga la Corona jumla ya mechi tano za Ligi Kuu England zimesimishwa kutokana na kuchukua  tahadhari dhidi ya Janga la Corona ikiwa ni pamoja na ile iliyotarajiwa kuchezwa Januari 13, kati ya Aston Villa dhidi ya Spurs.

Pia kikosi cha Aston Villa kwenye mchezo wa Kombe la FA dhidi ya Livelpool wakati ikipoteza kwa kufungwa mabao 4-1 kwenye Uwanja wa Villa Park ililazimika kuwatumia wachezaji wake chini ya miaka 23 na wale wa chini ya miaka 18 kucheza mchezo huo kutokana na baadhi ya wachezaji wao pamoja na wafanyakazi wengine kuwa na Corona.


KOCHA WA SIMBA KUIBUKIA GWAMBINA FC WATATU WATAJWA KURITHI MIKOBA YA SVEN SIMBA, MMOJA YUPO BONGO

Deprecated: File Theme without comments.php is deprecated since version 3.0.0 with no alternative available. Please include a comments.php template in your theme. in /home/sokalabo/public_html/wp-includes/functions.php on line 6170

Leave a Reply