Simba SC

LOKOSA IS RED..!!

admin January 25, 2021 2:45 pm


Simba SC leo Januari 25 wamemtambulisha rasmi mshambuliaji wao toka Nigeria, Junior Lokosa ambaye aliwasili nchini Jumamosi Januari 23.

Kupitia akaunti za mitandao ya kijamii ya Simba wamemtambulisha pamoja na kuweka picha zake akiwa ana saini mkataba.

Lokosa ni miongoni mwa wachezaji waliosajiliwa kwenye kipengele cha wachezaji watakaotumika hatua ya makundi ya Ligi ya Mabingwa Afrika ambapo Simba itakutana na AS Vita, Al Ahly na Al Merrikh.

Simba wameweka ujumbe unaosomeka “Chuma toka Nigeria na mchezaji wa zamani wa EspĂ©rance kipo tayari Msimbazi na dili lake yake limekamilika. Lengo kuu ni nusu fainali ya Ligi ya Mabingwa Afrika huku lengo mama likiwa Ligi Kuu na Kombe FA,”

Wameongeza kuwa “Simba Super Cup inakusubiri kwa hamu kubwa,”

Lokosa ataanza kuonekana kwenye mechi ya Simba Super Cup kuanzia Januari  27-31 jijini Dar.

TAIFA STARS HESABU ZOTE KWA GUINEA NGORONGORO HEROES WAPANGWA KUNDI LA KIFO AFCON

Deprecated: File Theme without comments.php is deprecated since version 3.0.0 with no alternative available. Please include a comments.php template in your theme. in /home/sokalabo/public_html/wp-includes/functions.php on line 6170

Leave a Reply