news

WALLACE KARIA APETA FIFA

admin January 28, 2021 10:47 am


 WALLACE Karia, Rais wa Shirikisho la Soka Tanzania,(TFF) amefanikiwa kuteuliwa kugombea nafasi ya Mjumbe wa Baraza la Shirikisho la Soka la Kimataifa (FIFA).

Nafasi ambayo amefanikiwa kuteuliwa Karia ni kwa nchi za Afrika zinazozungumza Lugha ya Kingereza.

Jina lake limepitishwa kugombea nafasi hiyo baada ya kufuzu kwenye kigezo cha uhakiki wa uadilifu, ukaguzi ambao hufanywa na Kamati Maalumu ya FIFA kwa wagombea wa nafasi mbalimbali ndani ya Shirikisho hilo.

Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na TFF, uchaguzi huo unatarajiwa kufanyika mwezi Machi 2021 nchini Morocco na Tanzania itawakilishwa na Karia. 

MZIMBABWE WA SIMBA ATAKA NAMBA KIKOSI CHA KWANZA MORRISON:WANASEMA NINA HERNIA, NITAFANYA KAZI SIMBA

Deprecated: File Theme without comments.php is deprecated since version 3.0.0 with no alternative available. Please include a comments.php template in your theme. in /home/sokalabo/public_html/wp-includes/functions.php on line 6170

Leave a Reply