YAN

YANGA WATAJA SABABU ZA MWANANCHI MEDIA DAY

admin February 2, 2021 3:47 pm


 MSHAURI ndani ya Klabu ya Yanga kuelekea kwenye mfumo wa mabadiliko, Senzo Mazingisa leo Feburuari 2, 2021 ametaja sababu tatu za klabu yao kuandaa siku maalum ya vyombo vya habari katika kambi yao ya AVIC Town iliyopo Kigamboni jijini Dar es Salaam.

 

Senzo amesema sababu ya kwanza ni kutoa fursa kwa wanahabari kujua na kuzungumza mambo ya mahusiano kati ya klabu yao na wadhamini wao.

 

“Siku zote Yanga ikicheza nafasi ya kuzungumza huwa kwa makocha, wachezaji wanafanya vizuri na kama ukiwa na bahati utaongea na nahodha.


“Leo ni tofauti nawaona wawakilishi wa wadhamini wetu SportPesa, GSM, Afya, Taifa Gas muwaulize leo kwanini wanaidhamini Yanga na kuendelea kuwapa pesa.

 

“Senzo amesema sababu ya pili ni kutoa nafasi kwa waandishi kujua mazingira ya kambi yao iliyopo Kigamboni na kujua mazingira yake na tatu ni kuzidisha umoja kati ya Yanga na Waandishi wa Habari na kuwa karibu na mashabiki,” .


JESHI LA KLABU YA AZAM DHIDI YA TP MAZEMBE LEO JONAS MKUDE AREJEA MAZOEZINI BAADA YA KUKOSA MECHI NANE

Deprecated: File Theme without comments.php is deprecated since version 3.0.0 with no alternative available. Please include a comments.php template in your theme. in /home/sokalabo/public_html/wp-includes/functions.php on line 6170

Leave a Reply