Taifa Stars

ISHU YA NDAYIRAGIJE KUCHIMBISHWA STARS NGOMA NZITO

admin February 10, 2021 12:47 pm


 IKIWA tetesi zinaeleza kuwa Ettiene Ndayiragije, Kocha Mkuu wa timu ya Taifa ya Tanzana, Taifa Stars amesitisha mkataba wake, Shirikisho la Soka Tanzania,(TFF) limesema kuwa lina utaratibu maalumu wa kutoa taarifa.

Ndayiragije alishindwa kukiongoza kikosi cha Stars nchini Cameroon kutinga hatua ya robo fainali kwenye mashindano ya Chan ambayo yanawahusu wachezaji wa ndani nchini Cameroon.

Kutokana na kuboronga huko inaelezwa kuwa amechimbishwa ndani ya Stars ili kuweza kumpata kocha mpya ambaye atakuwa ndani ya Stars.

Stars ilikusanya pointi nne baada ya kucheza mechi tatu, ilishinda moja, sare moja na ilichapwa mechi moja ya ufunguzi kwa mabao 2-0.

Kombe la Chan limekwenda tena nchini Morocco ambao walikuwa ni mabingwa watetezi wa taji hilo ambalo walilitwaa 2018 na kulifanya taifa hilo kutwaa taji hilo mara mbili.

KAGERE AANDIKA HISTORIA MBELE YA AZAM BWALYA: NITALIPIZA KISASI KWA SIMBA

Deprecated: File Theme without comments.php is deprecated since version 3.0.0 with no alternative available. Please include a comments.php template in your theme. in /home/sokalabo/public_html/wp-includes/functions.php on line 6260

Leave a Reply