Simba SC

SIMBA WATUA DR CONGO KAMILI KUIVAA AS VITA

admin February 10, 2021 1:47 pm


WAWAKILISHI wa Tanzania kwenye Ligi ya Mabingwa Afrika, Simba leo Februari 10 wamewasili salama Kinshasha, DR Congo kwa ajili ya maandalizi ya mwisho ya mchezo wao dhidi ya AS Vita.

Simba chini ya Kocha Mkuu, Didier Gomes ilianza safari jana, Februari 9 kwa kutoka Dar na kuweka kambi ya muda Addis Ababa na leo asubuhi walianza safari kuwafuata wapinzani wao.

Mchezo huo wa kwanza kwa Simba iliyo kundi A unatarajiwa kuwa na ushindani mkubwa kwa timu zote kwa kuwa zinatambuana vema hasa baada ya kuwahi kukutana mara mbili msimu wa 2018.

 Mchezo wa kwanza ambao ulichezwa Congo, Simba ilifungwa mabao 5-0 na AS Vita walipokuja Uwanja wa Mkapa walipoteza kwa kufungwa mabao 2-1 na Simba iliweza kutinga hatua ya robo fainali.

Gomes amesema kuwa wanakwenda wakiwa na kazi ya kusaka ushindi kwenye mchezo huo hivo wanaamini watafanya vizuri ndani ya dakika 90.

“Tunahitaji kuona tunafanya vizuri mchezo wetu wa kimataifa, tutapambana ili kupata matokeo na hilo linawezekana,” .

Nyota Jonas Mkude ambaye alikuwa nje ya uwanja kwa muda kutokana na utovu wa nidhamu naye ni miongoni mwa wachezaji ambao wapo kwenye msafara huo.

YANGA KUIFUATA MBEYA CITY NA WACHEZAJI 24, SAIDO ABAKI BONGO KOCHA SIMBA AWAANDALIA AS VITA SAPRAIZI

Deprecated: File Theme without comments.php is deprecated since version 3.0.0 with no alternative available. Please include a comments.php template in your theme. in /home/sokalabo/public_html/wp-includes/functions.php on line 6170

Leave a Reply