Azam FC

AZAM WATAJA SABABU ZA KUPOKEA KICHAPO MBELE YA COASTAL UNION

admin February 12, 2021 7:47 am


UONGOZI wa Azam FC umesema kuwa haukuwa na chaguo la kufanya Uwanja wa Mkwakwani jana kwa kuwa uwanja haukuruhusu wacheze mipira ya chini jambo ambalo liliwafanya wapoteze pointi tatu.


Azam FC inayonolewa na Kocha Mkuu, George Lwandamina ilikubali kuacha pointi tatu zote baada ya kufungwa mabao 2-1.

Ofisa Habari wa Azam FC, Zakaria Thabit amesema kuwa aliongea na mwalimu na kumuuliza tatizo lipo wapi mwalimu aliweka wazi kwamba uwanja ulikuwa tatizo kwao kuwa haukuruhusu mipira ya chini.

“Haukuwa uwanja rafiki kwetu kwa kuwa ulikuwa hauruhusu mipira ya chini jambo ambalo limetufanya tushindwe kupata matokeo chanya ndani ya uwanja.

“Ukiangalia kwa takwimu vijana wetu walipambana na kufanya vizuri ila wapinzani wetu waliweza kupiga mashuti mawili yaliyolenga lango na wakashinda hivyo tunajipanga kwa ajili ya mechi zijazo,”.
 
NYOTA WAZAWA WAWILI WAONGEZA AKAUNTI ZA MABAO,TIMU ZAO ZAGAWANA POINTI KOCHA SIMBA: NAMJUA VIZURI IBENGE, NINAJIAMINI

Deprecated: File Theme without comments.php is deprecated since version 3.0.0 with no alternative available. Please include a comments.php template in your theme. in /home/sokalabo/public_html/wp-includes/functions.php on line 6170

Leave a Reply