Ligi Kuu

BARAZA ASEPA NA TUZO YA KOCHA BORA BONGO

admin February 12, 2021 4:47 pm


 FRANCIS Baraza, Kocha Mkuu wa Klabu ya Biashara United ameibuka na tuzo ya kocha bora kwa mwezi Januari ndani ya Ligi Kuu Bara kwa mujibu wa Kamati ya Tuzo ya VPL.

Baraza ametwaa tuzo hiyo baada ya kuwashinda Charles Mkwasa wa Ruvu Shooting na Abdalah Mohamed,’Bares’ wa JKT Tanzania.

Kwa kutwaa tuzo hiyo anaungana na kocha wa Yanga, Cedric Kaze ambaye ametwaa tuzo hiyo mara mbili kwa mwezi Oktoba na Desemba huku Aristica Cioaba aliyekuwa Azam FC akitwaa tuzo hiyo Septemba.

Mkwasa alitwaa tuzo hiyo Novemba na kuwa mzawa wa kwanza ndani ya msimu wa 2020/21 kutwaa tuzo hiyo kwa upande wa makocha.

Pia nyota Deogratius Mafie, mshambuliaji wa Biashara United ametwaa tuzo ya mchezaji bora akiwashinda wachezaji wenzake ambao ni Mohamed Issa wa Ruvu Shooting na Wallace Kiango wa Mwadui FC.

Wengine ambao wameshawahi kutwaa tuzo hiyo ni pamoja na Prince Dube wa Azam FC mwezi Septembe,Tonombe Mukoko wa Yanga Oktoba John Bocco wa Simba Novemba na Saido Ntibazonkiza wa Yanga Desemba.

LIGI IMEGAWANYIKA KWA SASA VIPANDE VITATU RUVU SHOOTING YATULIZWA MBELE YA IHEFU,YAPIGWA 2-0

Deprecated: File Theme without comments.php is deprecated since version 3.0.0 with no alternative available. Please include a comments.php template in your theme. in /home/sokalabo/public_html/wp-includes/functions.php on line 6170

Leave a Reply