news

HIMID MAO ATUA ENTAG EL HARBY YA MISRI

admin February 6, 2021 8:47 am

 

KIUNGO wa kimataifa wa Tanzania, Himid Mao ‘Ninja’ amekamilisha dili la kujiunga na Entag El Harby FC inayoshiriki Ligi Kuu ya Misri akitokea Enppi FC.

Himid amejiunga na klabu hiyo akiwa mchezaji huru, kufuatia mkataba wake na Enppi kufikia kikomo mwishoni mwa msimu uliopita.Himid anakuwa mchezaji wanne kusajiliwa na Entag El-Harby SC akitanguliwa na Ahmed Saber pia kutoka Enppi, Mohamed Sosta kutoka Aswan na kipa Ahmed Busca.

 Entag El-Harby SC imekuwa na mwanzo mbaya katika msimu huu, hali iliyosababisha kuburuza mkia kwenye msimamo wa ligi hiyo, ikiwa na alama tano tu, baada ya kucheza michezo tisa, hivyo kusababisha kocha mkuu wa timu hiyo, Mokhtar Mokhtar kutimuliwa kazi.

 Himid Mao alianza kucheza soka Misri mnamo Julai 2018, akisajiliwa na Petrojet, lakini mwaka mmoja baadaye alihamia Enppi, akiichezea michezo 22 msimu uliopita.

KUMUONA FISTON WA YANGA BUKU TATU CHIKWENDE: AZAM WASUBIRI MOTO WANGU KESHO KWA MKAPA

Deprecated: File Theme without comments.php is deprecated since version 3.0.0 with no alternative available. Please include a comments.php template in your theme. in /home/sokalabo/public_html/wp-includes/functions.php on line 6170

Leave a Reply