Yanga SC

YANGA: TUKO TAYARI KUWAVAA COASTAL

admin March 3, 2021 4:47 pm


KIKOSI cha klabu ya Yanga leo kimefanya mazoezi yao ya mwisho kuelekea mchezo wao wa kesho dhidi ya Coastal Union huku wakitamba kufanya vizuri katika mchezo huo.

Mchezo huo unatarajiwa kupigwa katika dimba la Mkwakwani, jijini Tanga majira ya saa 10 kamili jioni.

Yanga wametamba kuwa, ushindi wa bao 1-0 walioupata kwenye mchezo uliopita dhidi ya Kengold, katika michuano ya kombe la Shirikisho umezidi kuamsha ari ya kushinda mchezo wa kesho.

Akizungumzia maandalizi yao kuelekea mchezo huo, Ofisa Mhamasishaji wa Yanga, Antonio Nugaz amewaomba Wanayanga kujitokeza kwa wingi, ili kuwapa sapoti wachezaji wa kikosi hicho.

“Kikosi chetu kimekamilisha mazoezi ya mwisho leo kuelekea mchezo wa kesho dhidi ya Coastal Union.

“Ni wazi ushindi tulioupata katika mchezo uliopita dhidi ya Kengold kwenye michuano ya kombe la FA, umezidi kutupa ari ya kufanya vizuri kwenye mchezo huu,”

MONALISA AANZA NA MIKWARA SIMBA QUEENS MANULA AFUNGUKA HAYA KUHUSU TUKIO ZIMA LA KUZIMIA UWANJANI

Deprecated: File Theme without comments.php is deprecated since version 3.0.0 with no alternative available. Please include a comments.php template in your theme. in /home/sokalabo/public_html/wp-includes/functions.php on line 6170

Leave a Reply